Wednesday, June 22, 2011

Waziri Mkuu Mstaafu, John Samuel Malecela hali yake si nzuri kiafya

Waziri Mkuu Mstaafu, John Samuel Malecela yupo taabani, amefanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo.

Spika wa Bunge la Jmhuri ya Muungano wa Tanzania, Anna Makinda aliwatangazia wabunge jana kabla ya kuahirisha kikao cha asubuhi kuwa Malecela ni mgonjwa.

Alisema, Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela haonekani bungeni kwa sababu Mzee Malecela ni mgonjwa. Kilango ni mke wa ndoa wa mzee Malecela.

“Waheshimiwa wabunge kwa siku kadhaa mheshimiwa Anne Kilango haonekani, yupo anamuuguza mzee Malecela kwa sababu amefanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo,” alisema spika leo.

Hata hivyo, Spika Makinda hakueleza hali ya Malecela inaendeleaje, kama ana nafuu ama la.

Source: Global Publishers Tz

No comments:

Post a Comment