Friday, July 25, 2014

DOUBLE RELEASE YA ALI KIBA: Mwana / Kimasomaso


Baada ya wapenzi wa muziki Tanzania kusubiri kwa muda mrefu sasa wamepata nafasi ya kujiburudisha na ngoma mpya kutoka kwa Alikiba. Tarehe 25 Julai, 2014 Alikiba ameachia single mbili mpya kwa wakati mmoja ziitwazo “Mwana” na “Kimasomaso”. Alikiba anajulikana ndani na nje ya Tanzania kwa hit zake kama Cinderella, Mapenzi yanarun dunia, Single boy, na Dushelele. Cinderela ndiyo wimbo ambao mpaka sasa umeweka rekodi ya kuuza copy nyingi katika Afrika Mashariki mwaka 2008. Mwaka 2012 Alikiba alishinda tuzo ya best Rhumba/ Zouk na wimbo wake wa “Dushelele” katika tuzo za Kilimanjaro Tanzania Music Awards. Alikiba anajulikana kwa uwezo wake mkubwa wa kuimba na utunzi wa nyimbo pamoja na kuwa mburudishaji mkali sana katika show zake za live na mpaka sasa ametembea nchi nyingi sana duniani kuburudisha wapenzi wa muziki. Sasa unaweza kupata nyimbo mbili mpya za Alikiba katika tovuti ya www.mkito.com

No comments:

Post a Comment