

Shoo hiyo, ‘itagemuliwa’ na Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, huku wakongwe Haroun Kahena ‘Inspector Haroun’ na Karama Bakari ‘Luteni Kalama’ wakiwa na dhamira ya kuthibitisha kwamba Gangwe Mob Bongo jukwaani ni sawa na G Unit Marekani.
Shujaa wa Kundi la Wagosi wa Kaya, Fred Maliki ‘Mkoloni’, Anselm Ngaiza ‘Soggy Dog’ na mwana Hot Pot Family mwenzake, Suma G, Mapacha, Dani Msimamo, G Solo, Rama Dee, Peen Lawyer, Adili Mkwela ‘Hisabati’, D wa Geto, Magazijuto, Coin, LWP ‘Majitu’ na wengine kibao.
Uchunguzi umebaini kuwa gumzo kuhusu shoo hiyo imeshika mbaya kitaani, huku ubunifu wa matangazo na viwango vya Vinega wa Anti Virus vikiwa ni kielelezo cha kumfanya kila Mtanzania aone tamasha hilo si la kukosa.
Mratibu wa shoo hiyo, Mkoloni anapatikana kwa namba 0719 690 100, hivyo maelezo kuhusu utaratibu wote kwa jumla, yanapatikana kwake.
Na GlobalPublishersTz
No comments:
Post a Comment